MCHUNGAJI MGAMBO ASHAURI SERIKALI KUSIMAMIA MAADILI.

Leonce Zimbandu

MCHUNGAJI wa Kanisa la Free Pentecoste  (FPCT)  Majohe Bwela, David Mgambo ameishauri serikali kuendelea kusimamia 
maadili bila kubagua vyama vya siasa wala dini ili kuendelea kudumisha amani.

Ushauri huo umetolewa  na Mchungaji Mgambo wakati wa  mahubiri kwenye mkutano  wa siku saba  wa Injili unaoendelea katika viwanja vya kanisa hilo wenye lengo la watu wamjue mungu ili  kuepuka uovu.

Amesema  serikali  hupambana na uhalifu kwa kutumia vyombo vya dola lakini watumishi wa Mungu hushughulikia  uovu kwa kuhubiri neno la Mungu  kwa watu wote ili waachane  na uhalifu katika jamii.

“Unajua sisi ni watendakazi wa serikali ya mbinguni lakini  vyombo vya dola vinafanyakazi  kwa kutumia nguvu na sheria za kidunia, hivyo tukishirikiana tutafanikiwa kutokomeza uhalifu,” alisema.

Aidha, Mchungaji Mgambo amesema  pamoja na Kanisa la FPCT kufanya kampeni hiyo  Septemba  kila mwaka na  lakini yeye alikuwa akiendelea kumuomba mungu  ili aepushe  mauji ya watu wasio na hatia  yaliyotokea kule Kibiti, Lindi na Mkurunga.

Aliendelea kusisitiza kuwa   maombi ya watumishi wa Mungu katika matukio yaliyotokea nchini yameisaidia serikali kudhibiti  kwa haraka ili kudumisha  amani yetu iliyodumu kwa miongo mitano sasa.





Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL