MAPIMAMATA WALIOMBA JESHI LA POLISI KUFANYA UKAGUZI.


Na Mwandishi Wetu.

CHAMA cha Maendeleo ya Madereva Pikipiki Matairi Matatu Tanzania (MAPIMAMATA),  kimeliomba Jeshi la Polisi Nchini kufanya ukaguzi  kwenye vituo  vya madereva bajaji ili kubaini bajaji zinazoibiwa.

Akizungumza na mwandishi wa blog hii leo Mwenyekiti wa chama hicho, Edward Mwenisongole  amesema zaidi ya bajaji 10 zimeibiwa ndani ya mwezi mmoja na madereva wawili kuuwawa na hakuna hatua yeyote inayochukuliwa.



Mwenisongole, amesema changamoto hii ya kuibiwa hawaoni juhudi yeyote ya kusaidiwa maana wanaamini hizo bajaji zinazoibiwa zinafanya kazi baadhi ya maeneo.

“Tunaliomba Jeshi la Polisi Nchini lifanye ukaguzi kwenye vituo vya madereva wa bajaji ili kubaini bajaji zinazoibiwa hii ni kutokana na wizi unaoendelea na kugharimu maisha yetu,”anasema Mwenisongole

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL