MILIONI 800 ZATENGWA ILALA KUJENGA MATUNDU YA VYOO.


Leonce Zimbandu

MANISPAA ya Ilala inatarajia kutoa  sh. Milioni 65.5 kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya choo 16 katika Shule ya msingi Bunge  ili kutatua   changamoto ya miundo mbinu  iliyodumu kwa muda mrefu.

Kati ya pesa tayari sh. Milioni 20 zimetolewa kwa ajili ya kukamilia sakafu ya chini yenye jumla ya matundu manane na ujenzi wa sakafu hiyo unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi huu.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Manispaa ya Ilala, Tabu Shaibu aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  ofisini kwake leo.

Amesema uamuzi wa kujenga choo cha ghorofa katika shule ya Msingi Bunge umetokana  na hali halisi ya  ufinyu wa eneo lenyewe, hivyo serikali itajenga sakafu mbili, sakafu ya chini matundu manane na juu matundu manane.

“Unajua juhudi za serikali kutatua changamoto zinaendelea kwa kutenga fedha kila mwaka kwenye bajeti, kwa mwaka 2017/2018 Manispaa ya Ilala imetenge sh. Milioni 800 kwa ajili ya matundu ya vyoo 400,” alisemaTabu.
Manispaa imetenga fedha hizo kutoka kwenye vyanzo vyake vya mapato ya ndani na fedha za maendeleo ya serikali za mitaa (LCDG), pia wadau wanaendelea kuchangia katika ujenzi wa matundu hayo.


Aidha, Tabu ameendelea kusema kuwa pamoja matundu yaliyopo ya vyoo laki kutakuwa na chumba maalumu cha watoto wa kike na walemavu ili kuepusha usumbufu.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL