ACT- WAZALENDO CHAWAKANA VIJANA WALIOJIUNGA CCM

Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam Salum Sudi (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukana vijana wane walioamia chama cha Mapinduzi (CCM) na kujitambulisha kuwa walikuwa viongozi ndani ya ACT ambapo mwenyekiti huyo  alisema siyo kweli hawakuwa viongozi, kulia ni Katibu Kata ya Kijichi Sadick Mussa (kushoto) Hassan Mchinya Katibu Mwenyezi Mkoa wa Dar es Salaam na Eliamin Kantu Mwenyekiti wa Vijana Kata ya Kijichi (Na Mwandishi wetu)


Na Mwandishi Wetu.

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimewakana vijana wanne waliojiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM), ambapo vijana hao wakati wakijinadi kwenye mkutano wa Kampeni za Udiwani zilizokuwa zinafanyika  Mwanamtoti Kata ya Kijichi Novemba 12, 2017, walisema kuwa wakati wako ACT walikuwa ni viongozi ambapo chama hicho kimesema siyo kweli kwamba walikuwa ni viongozi badala yake walikuwa ni wanachama wa kawaida.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam Salum Sudi, wakati akizungunza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam,  kuhusu kukana wanachama hao kwamba siyo kweli kwamba walikuwa ni viongozi.

Mwenyekiti Sudi, aliwataja vijana hao kuwa ni Hassan Massamaki aliyejitambulisha kama Katibu Kata ya Kijichi, Ally Kera alijitambulisha kama Mwenyekiti wa Vijana Kata ya Kijichi, Elia Kihoza alijitambulisha kama Mwenykiti wa Vijana Kata na Kijana Azizi Mukaka alijitambulisha kama Mhekahazina.

"Hawa vijana ni wahongo, ukweli ni kwamba hawakuwa viongozi ndani ya ACT-Wazalendo badala yake walikuwa ni wanachama wa kawaida, ifike watu wawe wanasema ukweli kwani hakuna mtu anayemkataza mwanachama kuamia chama kingine ni mapenzi ya mtu lakini siyo kwamba mtu aseme uongo ili kujikweza,"alisema Mwenyekiti Sudi.

Alisema ni vyema baadhi ya watu ambao wanaamua kujiunga na vyama vingine ni vyema wakachunguzwa kutokana na kwamba wamekuwa wakiviongopea vyama hivyo kwamba wao waliwahi kushika nyadhifa mbalimbali kumbe siyo kweli.

"Kwa mfano vijana hawa hakuna aliyewahi kuwa kiongozi hata mmoja hivyo wakati wakijinadi kwenye mkutano wa kampeni walisema kuwa wao walikuwa ni viongozi  kwa nyadhifa mbalimbali kumbe siyo kweli,"alisema Sudi.

Alisema tangu mwaka jana vijana hao walifukuzwa ndani ya chama cha ACT-Wazalendo walikuwa wanachama awali na si viongozi na wengi wamekuwa wakilagai sana wakati wakitaka kujiunga na vyama vingine.

Mbali na hilo pia alisema kuwa lipo tatizo la mgombea Udiwani wao Kata ya Kijichi anayejulikana kwa jina la .....  amekuwa akipata vitisho mbalimbali ambapo mbali na hilo analiomba Jeshi la Polisi kuingilia kati kutokana na kwamba mgombea huyo tayari ameisha pata hasara ya kuchomewa shule yake na kusema kuwa upo umuhimu wa kufanya kampeni za kistarabu tofauti na hali ilivyo sasa.

Katibu wa ACT-Wazalengo Kata ya Kijichi Sadick Mussa, alisema kuwa wamejipanga vya kutosha kuhakikisha wanashinda uchaguzi huo na si vinginevyo na kusema kuwa wananchi wasiwe na wasiwasi kuhusiana na kuibuka kidedea.







Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL