CHANGAMOTO YA USAFIRI INAVYOKITESA KITUO CHA SIFA.

 Mwazirishi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha  Sifa Group ambaye pia ni Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Nchini, Sifa John, akielezea jinsi Mungu alivyomuita kwaajili ya kulea watoto yatima ambapo hadi sasa kituo hicho kina watoto 50.

 Mtumishi wa Mungu na Mwalimu Alice Haule akizungumza na Mwazirishi wa kituo chicho Sifa John baada ya kuwasili katika kituo hicho kwaajili ya kutoa misaada na kuwafariji watoto hao.


 Watoto Yatima wa Kituo cha Sifa Group wakiwakaribisha wageni hawapo pichani waliowatembelea kwaajili ya kutoa misaada mbalimbali pamoja na kuwafaliji.

 Muimbaji wa Nyimbo za Injili na Producer Testimony akiongoza sala kabla ya kuondoka kwenye kituo hicho.



 Mtumishi na Mwalimu Alice Haule kulia akiwa na picha ya pamoja na Mwazilishi wa kituo hicho Sifa John kushoto.

 Mtumishi na Mwalimu Alice Haule akiwa  na familia yake akiwa na picha ya pamoja na Mwazirishi wa kituo hicho.

 Mchungaji Mkuu  wa Kanisa la Christian Life Eliya Peter, ambapo miongoni mwa waumini wake waliongozana na familia ya Mtumishi na Mwalimu  Alice Haule kwaajili ya kwenda kutoa misaada kwa watoto hao na kuwafaliji.

Mtumishi Mungu na Mwalimu Alice Haule akizungumza na Mwazirishi wa kituo hicho Sifa baada ya kuwasili kituoni hapo jana jioni.

Enles Mbegalo

Mwazirishi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha  Sifa Group ambaye pia ni Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Nchini, Sifa John, amewaomba watu wenye mioyo ya utoaji  na Taasisi mbalimbali kumsaidia kuboresha miundombinu ya barabara kwenye kituo  hicho kilichopo Vikawe Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Hayo aliyasema jana wakati familia ya  Mtumishi wa Mungu na Mwalimu Alice Haule pamoja Muimbaji wa Nyimbo za Injili na Producer Testimony  na mke wake na  baadhi ya waumini kutoka  Kanisa la Christian Life, lililopo Tegeta Nyuki jijini Dar es Salaam, linalosimamiwa na Mchungaji Mkuu  Eliya Peter waliotembelea kituo hicho na kutoa misaada mbalimbali.

Sifa alisema kutokana na ubovu wa miundombinu iliyopo kwenye kituo hicho hulazimika  kutumia Shilingi 30,000  kwa  siku kwaajili ya usafiri.

“Changamoto kubwa iliyopo  katika kituo changu ni  usafili wa watoto kuwatoa hapa kituoni hadi shuleni kwani watoto wanasoma Bunju na  nalazimika kutoa Shilingi 30,000 kwa siku kwaajili ya  usafili wa gari dogo ambalo tunakodi kwaajili ya kuwapeleka watoto hawa shuleni na kuwarudisha,” amesema

Hata hivyo alisema changamoto nyingine  ni chakula, Sre za Shule pamoja na maji, ingawa tatizo la maji limetatuliwa kwa kiasi kidogo.

Naye Alice Haule alisema aliguswa na watoto hao na kumua kwenda kupeleka misaada mbalimbali ikiwamo malazi, chakula na vitu mbalimbali.

Pia Mtumishi wa Mungu Alice amesema amekuwa akihudumia kituo hicho kwa kipindi cha miaka mitano sasa.

Kwa yeyote atakayeguswa na kutaka kuwasaidia watoto hawa awasiliane na Sifa John kwa namba za simu  0652 562348 na 0766 913780



Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL