MAELFU YA WAKAZI DAR WATUMIA IPASAVYI FURSA YA RC MAKONDA YA UPIMAJI NA MATIBABU BURE NDANI YA MELI YA CHINA.


 *Maelfu ya Wananchi wa Dar es Salaam Leo wamejitokeza kwa wingi* kuchangamkia fursa ya *Upimaji na Matibabu Bure ndani ya Meli ya Jeshi la Jamuhuri ya China* ambapo katika Hali isiyotarajiwa wananchi kutoka *Mikoani na Nje ya Jumuiya ya Africa Mashariki wamesafiri kuja kufuata huduma hiyo.*

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. PAUL MAKONDA* amewatembelea wananchi hao na kusema *kila atakaefika na kupatiwa kadi atapatiwa vipimo, matibabu na dawa Bure* na kuwaasa wananchi kutumia vyema fursa hiyo.

 *RC MAKONDA* amesema Madaktari wengine wa China wanaendelea na huduma za matibabu kwenye *Hospital za Muhimbili, MOI, Ocean Road, Mwananyamala, Amana na Temeke* ili kuhakikisha wanahudumia idadi kubwa ya wananchi.

Amesema *hadi kufikia majira ya mchana tayari wagonjwa 516 walikuwa wamepimwa na kupatiwa matibabu* jambo linaloonyesha kuwa wananchi wote watapatiwa huduma.

 *MAKONDA* amesema *wapo madaktari bingwa maalumu waliobobea kwa kutoa dawa za kichina* kwa wale wagonjwa ambao dawa nyingine zimekuwa zikishindwa kutibu.

Amesema lengo ni kuhakikisha *hakuna mtu anaepoteza maisha kwa kigezo cha kukosa huduma au kumudu gharama.*

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL