MOROVIANI UKONGA YAJIPANGA KUJENGA MAADILI KWA VIJANA

 Goodluck Michael akibatizwa katika ibada ya Jumapili jana, katika kanisa la Morovian Ukonga .


Ibada ya ubatizo na kipaimara  ikiendelea katika kanisa la Moroviani Ukonga iliyofanyija jana.

 Kwaya ya Ustawi wa Jamii wakitumbuiza kwenye ibada hiyo jana.


 Mwandishi wa Habarai wa Upendo Radio Michael Malanyi akiwa kwenye picha ya pamoja na familia yake baada ya ibada .

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Morovian Ukonga , Samweli Mwambopo kulia  na Wachungaji wenzake wakizungumza na  waandishi wa habari baada ya kumaliza ibada ya jana.

Michael Malanyingi

MCHUNGAJI Kiongozi wa Kanisa la Moraviani Ushirika wa Ukonga, Samwel Mwambopa amesema Kanisa  limejipanga kuwajengea uwezo vijana kwa  kuwafundisha   maadili ya kikristo, yakiwamo mafundisho ya ubatizo na kipaimara. 

Kauli hiyo imetolewa na Mchungaji huyo kwenye ibada ya ubatizo na kipaimara iliyofanyika katika Kanisa hilo  mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Alisema  mafundisho ya vijana hao 20 yalitolewa kwa muda wa mwaka mmoja kwa lengo la kuwajenga na kuimarisha kiimani ya kikristo ili kulinda maadili ambayo yapo hatarini kutoroka.

“Unajua vita dhidi ya ufisadi ni matokeo ya mmomonyoko wa maadili, hivyo tunahitaji kurudisha maadili kwa vijana ili kukomesha vitendo hivyo,” alisema.

Alisema kanisa, wazazi na walezi wanaendelea kujipanga  kuhakikisha elimu iliyotolewa kwa vijana hao inaendelezwa na kudumisha maadili mema katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Mchungaji wa Kanisa la Sayuni toka Boko ambaye aliongoza ibada hiyo ya Kipaimara, Mwigane Mwakalinga alisema iwapo maadili hayo yataendelezwa, usanii ndani ya kanisa utaondoka.

Alisema kila mkristo anapaswa kujiandaa kabla hajafika kwenye madhabahu ya mungu kwa vile anapatikana kwenye sifa, hivyo hata waimbaji wa nyimbo za injili wanapaswa kujiandaa na kuonesha heshima mbele  ya madhabahu.

“Unajua waimbaji wengi hujisahau wanapotoa huduma ya uimbaji kwenye madhabahu, wanatakiwa kujiandaa na kunyenyekea wakati wa kutoa huduma,” alisema.

Aliongeza kuwa wengi wanabadilisha hata staili ya nywele zao na hata mavazi yao, hivyo kanisa litahakikisha usanii wa aina hiyo unarekebishwa ili kufuata maadili ya kanisa na siyo ya kisanii.

Mmoja wa wazazi wa watoto waliopata ubatizo,Amisa Joseph alisema kuwa yeye kama mzazi wa Goodluck Michael atahakikisha  mtoto wake anaendelea kukua katika maadili mema.

“Tunaendelea kumwomba mungu atusaidie ili kulea familia yetu katika njia ziwapasazo za kikristo,” alisema.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL