RC LUHUMBI ASISITIZA WANANCHI KUTUMIA RASILIMALI WALIZONAZO KUCHOCHEA MAENDELEO
Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita akishiriki kuchanganya mchanga kwenye shughuli ya ujenzi wa zahanati katika kijiji cha Kazibizyo wakati wa zoezi la uhamasishaji wananchi kujitolea katika uchangiaji wa maendeleo ya ujenzi wa zahanati,vituo vya afya na shule Wilayani Bukombe.
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe ambaye yupo (Katikakati)Josephat Maganga akishirikiana na wananchi pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kufanya shughuli ya kuchanganya mchanga.
Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita akishiriki kujenga msingi wa kujenga zahanati ya kijiji cha Kazibizyo Wilayani Bukombe pamoja na wananchi ambao wamejitokeza kuunga jitihada za serikali za kuleta maendeleo ya huduma za afya maeneo ambayo yanauwitaji .
Katibu tawala wa wilaya ya Bukombe akishiriki zoezi la ujenzi.
Wananchi wa kijiji cha Kazibizyo wakishiriki kusomba mawe.
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akiendelea na harakati za kushiriki ujenzi wa zahanati kijijini hapo.
Wakina mama wakishiriki zoezi la ujenzi wa zahanati kijiji cha Kazibizyo .
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe,Josephat Maganga akizungumza na wananchi wa kijiji hicho juu ya kujitolea kwenye swala la maendeleo bila ya kutegemea serikali.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kazibizyo baada ya kuzindua kampeni ya ujenzi wa zahanati kijijini hapo.
Comments
Post a Comment