VIJANA CHANGAMKIENI FURSA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI.

 Kiongozi wa  Umoja wa Vijana wa  Chama cha Mapinduzi ( UVCCM) Wilaya ya Kinondoni  ambaye pia ni Mshauri wa chama cha Madereva hao, David Massatu akizungumza na madereva hao baada ya kuwasili kwenye semina hiyo.



 Meza kuu wakifuatilia mmoja wa Maofisa  kutoka Kampuni ya Bajaji ya Sunbeam Auto, inayotoa mikopo ya bajaji  Mpya aina ya RE 4S kwa gharama nafuu, katikati ni  Kiongozi wa  Umoja wa Vijana wa  Chama cha Mapinduzi ( UVCCM) Wilaya ya Kinondoni  ambaye pia ni Mshauri wa chama cha Madereva hao, David Massatu, kulia ni Ofisa Maendeleo  ya Vijana Mkoa wa Dar es Salaam, Masalida Zephania Njashi  na kushoto ni Mwenyekiti wa  Chama cha Maendeleo ya Madereva Pikipiki Matairi Matatu Tanzania (Mapimamata), Edward Mwenisongole.
Baadhi ya madereva Bajaji wakifuatilia semina hiyo ya fursa mbalimbali kwa vijana   leo jijini Dar es Salaam.

 Madereva hao wakiendelea kufuatilia mafunzo mbalimbali yanayotolewa  kwenye semina hiyo leo.
 Mmoja wa maofisa kutoka Kampuni ya Bajaji ya Sunbeam Auto, inayotoa mikopo ya bajaji  Mpya aina ya RE 4S, akitoa ufafanuzi juu ya mikopo inayotolewa  na Kampuni hiyo.

Na Mwandishi Wetu.

OFISA Maendeleo  ya Vijana Mkoa wa Dar es Salaam, Masalida Zephania Njashi amewataka vijana  kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali ili waweze kujikwamua kimaendeleo.

Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua  semina ya siku moja ya kutoa elimu kwa madereva wa Bajaji Kituo cha Ukwamani  juu ya fursa za vijana zinazotolewa na serikali.

“Serikali hasa hii ya awamu ya Tano ya Rais John Pombe Magufuli  imekuwa ikitoa fursa nyingi kwa vijana lakini vijana wamekuwa hawatumii fursa hizi kwa kuwa hawapo kwenye makundi yaliyosajiliwa,”amesema
Aidha aliwataka vijana hao kujiunga katika makundi mbalimbali kupitia Chama Cha Maendeleo ya Madereva Pikipiki Matairi Matatu Tanzania (MAPIMAMATA)  ili waweze kujisajiri na kupata mikopo kupitia vikundi hivyo kwani wakisajiliwa na kutambulika kisheria ni rahisi kupata mikopo.

Hata hivyo aliwaomba  madereva hao   kuisaidie serikali kupaza sauti kuhusu matukio mbalimbali ya uharifu  ambayo yamekuwa yakitokea kwani wao kutokana na huduma wanayoitoa ni rahisi kuwatambua watu  hao.

Kawa upande wake Kiongozi wa  Umoja wa Vijana wa  Chama cha Mapinduzi ( UVCCM) Wilaya ya Kinondoni  ambaye pia ni Mshauri wa chama cha Madereva hao, David Massatu amesema maendeleo ya Mkoa wa Dar es Salaam yanawategemea vijana kwani wao ndio nguvu kazi ya Taifa.

Pia alisema atawakutanisha madereva hao na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ili aweze kutambua huduma wanazozitoa na kuwapa ushirikiano.

Naye Mwenyekiti wa  Chama cha Maendeleo ya Madereva Pikipiki Matairi Matatu Tanzania (Mapimamata), Edward Mwenisongole  amesema viongozi wa vyama vya siasa wamekuwa wakiwajengea chuki vijana na serikali kwani wao wamekuwa  wakitetea maslahi yao tu.

“Viongozi wa siasa wamekuwa hawazungumzii fursa zinazotolewa na serikali kwa vijana ila wamekuwa wakitetea maslahi yao tu, hizi fursa zilizopo serikalini wanasiasa wamekuwa  hawatuelezi zaidi ya kutujengee chuki tu,”amesema

Hata hivyo semina hiyo iliambatana na utoaji wa elimu kwa vijana na kujitambua na kutoa fursa ya mikopo ya gharama nafuu kwa Kampuni ya Bajaji ya Sunbeam Auto, inayotoa mikopo ya bajaji  Mpya aina ya RE 4S.



Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL