WAITARA AIPIGA MKWARA CCM KIVULE.

 Mwenyekiti wa CCM  Ilala, Ubaya Chuma akimdadi mgombea wa chama hicho Amos Angaya  kwenye uzinduzi wa kampeni  kivule, mwishoni mwa wiki.


Viongozi wa CCM toka mitaa mbali mbali, waliohudhuria kampeni hizo mwishoni mwa wiki.

 Baadhi ya wanachama waliohudhuria kwenye  kampeni hizo.


Mbunge wa Jimbo la Ukonga akimnadi mgombea wa chadema Nasoro Bihimba.

Baadhi ya wanachama wa Chadema waliohudhuria kwenye kampeni hizo mwishoni mwa wiki.

Tambwe Hiza akizungumza na wanachama wa Chadema hawapo pichani.

Leonce Zimbandu

TAMBO  za uchaguzi mdogo wa wenyeviti wa mitaa  katika Kata ya Kivule Jimbo la Ukonga zimeanza kutawala huku Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakihitaji kuurudisha mtaa huo mikononi mwao  na Chadema wakihitaji kuendelea kuushikilia.

Akizungumza wakati wa kuzindua kampeni hiyo mwishoni mwa wiki kwenye standi ya Mbondole, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala, Ubaya Chuma alisema kuwa watahakikisha wanarudisha heshima kwa kushinda uchaguzi huo.

Alisema wanachama wa CCM wanatakiwa kujiuliza kwa nini mtaa huo ulichukuliwa na Chadema, hivyo jibu likipatikana itakuwa rahisi kwao kutwaa ushindi mapema.

“Tumejipanga na timu yetu ya ushindi, hivyo letu tumezindua kampeni na kuwanadi wagombea wa mitaa mitatu na kuwaombea kura,” alisema.

Wakati CCM wakiendelea  na tambo hizo, Mbunge wa jimbo la Ukonga Mwita Waitara amewaasa wananchi na wanachama  kufanya kampeni za kistaarabu na kamwe wasikubali kutumika vibaya.

Alisema hataki vurugu itokee katika jimbo hilo kwenye uchanguzi wa wenyeviti wa mitaa mitatu ya Kata ya Kivule, ukiwamo mtaa wake wa kivule kati.

Mitaa mingine ni Bomba mbili, Kerezange huku Mtaa wa Magole ukisubiri uhakiki wa mipaka ili kubainisha wananchi hao wako Temeke au Manispaa ya Ilala.

“CCM wanapaswa kufanya kampeni za kistaarabu kwa vile jimbo na kata ya Kivule linaongozwa na Chadema, hivyo wanapaswa kuheshimu sheria na kanuni,” alisema.

Alisema CCM wanatoa ahadi ambazo wanataraji kuzifanya lakini Chadema ndani ya miaka miwili wanazungumzia mafanikio katika jimbo na mitaa mbali mbali.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL