BUSTANI YA WAZEE YA UPENDO YAZINDULIWA.
![]() |
![]() |
Baadhi ya viongozi wa serikali waliohudhuria kwenye uzinduzi wa Bustani ya Upendo wakishiriki mazoezi ya viungo na baadhi ya wazee wa Mtaa wa Sea View jana jioni jijini Dar es Salaam.
![]() |
![]() |
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Sea View Victor Muneni aliyevaa tisheti jeupe akizungumza na wazee wa Mtaa huo baada ya uzinduzi wa Bustani ya Upendo iliyozinduliwa jana jijini Dar es Salaam.
Wazee waliohudhuria uzinduzi huo wakijifunza juu ya matumizi ya mimea ambayo inatumika kama mapambo na pia inatumika kama dawa ya kutibu magonjwa mbalimbali ikiwamo Alovera.
![]() |
![]() |
Viongozi waliohudhuria uzinduzi huo akiwamo Diwani wa Kata ya Kivukoni Henry Massaba, wakiendelea kujifunza matumizi ya mimea ambayo inatumika kama mapambo na pia kama dawa.
![]() |
![]() |
Picha ya pamoja ya wazee wa Mtaa wa Sea View pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali waliohudhuria uzinduzi wa Bustani hiyo jana.
Afisa Tarafa Kariakoo, Christina Kalekezi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo akizungumza na wazee hao (hawapo pichani) baada ya kuzindua Bustani hiyo jana, kulia ni Diwani wa Kata ya Kivukoni Henry Massaba.
![]() |
![]() |
Wazee wakiendelea kuelimishwa faida za mimea ambayo hutumika kama mapambo na pia ni dawa zinazotibu magonjwa mbalimbali.
Na Enles Mbegalo
MTAALAMU
wa Saikolojia Zinat Fazal ameitaka jamii kuto wanyanyapaa wazee bali iwapende
ili wajifunze mambo mazuri kutoka kwao.
Hayo ameyasema jana jijini Dar es Salaam wakati wa
Uzinduzi wa Bustani ya Upendo itakayotumika kufanyia mazoezi kwa wazee wote wa Mtaa wa Sea view kila siku ya Jumamosi.
“Wazee wana dhamani tuwajali na tuwaheshimu kwani wao ndio
wametufikisha sisi hapa tulipo jamii inatakiwa isiwanyanyapae bali iwapende kwani
watajifunza mambo mengi mazuri kutoka kwao,”alisema na kuongeza
“Sisi wakati mwingine tunawadharau wazee kutokana na
uzee wao ila tunatakiwa kuwapa kipaumbele kwa kuwapenda na kuwaheshimu,”.
Fazal alisema lengo la kuanzisha bustani hiyo ni kuelimisha jamii kwamba wazee wana thamani ,wajaliwe,wapewe upendo na heshima.
Fazal alisema lengo la kuanzisha bustani hiyo ni kuelimisha jamii kwamba wazee wana thamani ,wajaliwe,wapewe upendo na heshima.
Naye Afisa Tarafa Kariakoo, Christina Kalekezi
ambaye alikuwa Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo alimpongeza Mtaalamu wa Saikolojia
Fazal kwa ubunifu huo ambao
utawasaidia wazee wote wa Mtaa wa Sea View kufanya mazoezi kila siku ya jumamos ili
kuimarisha viungo vyao.
“Niwaombe
wazee wangu tusaidiane kukielimisha kizazi cha sasa hivi kwani kimepoteza
kabisa dira ya utunzaji wa mazingira wakija hapa watajifunza mambo mengi kutoka
kwenu,”
Pia alimpongeza Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa
Sea View Victor Muneni kwa kushirikiana na Mtaalamu wa Saikolojia Zinat Fazal kwa kuweza kushauriana na kubuni Bustani hiyo ya Upendo













Comments
Post a Comment