KANISA LA PENTEKOSTE LIMEZIPONGEZA TAASISI ZINAZOSAIDIA WATOTO WANAOISHI MAZINGIRA HATARISHI.

 Emanuel kwaya toka Kanisa la Anglikana parish ya  Ukonga Mazizini wakitumbuiza kwenye tamasha la kuchangia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu hivi karibuni.
 Mzee Kiongozi wa Kanisa la Pentekoste Tanzania Parish ya Airport, Joel Ndutu akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo Pichani) baada ya tamasha la kuchangia watoto wamaosihi kwenye mazingira magumu.
Mkurugenzi wa  Taasisi ya Mkusikilize Msaidie Anaweza (MMA), Raphael Mwazyunga alizungumza na waandishi wa habari Hawapo pichani baada ya kufanikisha tamasha la watoto hao hivi karibuni katika Kanisa la Pentekoste Tanzania Parish ya Uwanja wa ndege.


Na Leonce Zimbandu

KANISA la Pentekoste Tanzania Parish ya Uwanja wa Ndege imeipongeza Taasisi  inayowasaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi wakiwamo waliotelekezwa na wazazi na jamii.

Pongezi hizo zimetolewa na Mzee Kiongozi wa Kanisa hilo, Joel Ndutu baada kufanyika kwa tamasha lililohusisha wadau ambao  walichangia  vitu ili kuhakikisha wapelekwa shule mwakani.

Ndutu aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliofika kwenye tamasha na kushuhudia tukio hilo lililofanyika katika Kanisa hilo hivi karibuni.

Alisema taasisi imefungua milango ya watu kutambua athari za kutelekeza watoto na matokeo yake watoto kuishi maisha hatarishi ambayo hayampendezi mungu.

“Kanisa tumefurahi kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Msikilize Msaidie Anaweza kufanya tamasha hilo katika kanisa hilo, hiyo ni hatua moja ya kuunga mkono juhudi za serikali,” alisema.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Msikilize Msaidie Anaweza (MMA), Raphael Mwazyunga alisema lengo la kuanzisha taasisi hiyo ni kuwasaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na hatarishi.

Alisema walianza kuingia mitaa na kufanikisha  kuwapata watoto 70 kati yao 36  wanaishi katika mazingira hatarishi lakini wengine wanaishi na mzazi mmoja  wa kike ambaye hawezi kujikimu kimaisha.

“Chanzo  cha kutelekeza watoto  mitaani kinatokana na  kusambaratika kwa ndoa, hivyo wanawake wanapaswa kupunguza hasira ili kulinda ndoa zao,” alisema.

Alisema ataendelea kushirikiana na harakati za kuunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuwachukulia hatua wanaume watakatelekeza watoto.




Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL