MADIWANI ILALA WAOMBA TARULA IVUNJWE IMESHINDWA KUTENGENEZA BARABARA.


Na Heri Shaaban

BARAZA la Madiwani manispaa ya Ilala imesema kuwa imeshindwa kufanya  kazi na Wakala wa Barabara Tarula kwa kuwa toka wapewe  jukumu na Serikali hadi leo amna barabara zilizojengwa na kupelekea kero kwa wananchi.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana katika kikao cha Baraza la Madiwani Ilala na Mwenyekiti wa Baraza hilo Naibu Kaimu Meya wa Ilala Omary Kumbilamoto.

Akizungumza katika baraza hilo Kumbilamoto alisema toka Serikali iwape mamlaka Tarula hadi leo amna barabara zilizojengwa ndani ya manispaa hiyo na kupelekea kero kubwa ikiwemo Barabara za Vingunguti ambapo kwa sasa magari yanashindwa kupita kutokana na kuwa na mashimo makubwa.

" Mimi kama Mwenyekiti wa kikao cha baraza la leo tumeshindwa kufanya kazi na Tarula kwani imekuwa jina tuu  na  kama kweli wapo basi  Serikali iwape fedha iweze kujenga Barabara za Halmashauri ambapo nyingi zimeharibika"alisema Kumbilamoto.

Alisema   ndani ya Manispaa ya Ilala kwa sasa vilio vikubwa ubovu wa barabara za wananchi ndio kero kubwa na madiwani hawana uwezo wa kutatua kero katika kata zao  Kutokana na posho zao nyingi kufutwa kubaki na mshahara ambao wanalipwa kila mwezi.

Akielezea kuhusu madiwani wa  Chama cha  Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kususa kikao cha baraza hilo na kutoka nje ya ukumbi wakiongozwa na Diwani wa Tabata Patrick Asenga.

Kumbilamoto alisema  walitaka kufahamu mazimio ya kikao kilichopita cha madiwani na  agenda ya yatokanayo katika Muhtasari  ilikuwa hawakuweka katika kabrasha hilo. 

Alisema baadhi ya mambo mengine ambayo walitaka kuuliza yatokanayo ni swali alilouliza Diwani wa Kata ya Kipawa Kennedy Saimoni kutaka kujua matumizi ya fedha Mfuko wa Jimbo la Segerea hata hivyo alikupata majibu.

Kwa upande wa Diwani wa Viti Maalum Ilala Saada Mandangwa(CCM) katika baraza hilo aliwanyima nafasi Madiwani wa CHADEMA waliokuwa wakitaka  kumburuza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Palela Msongole wakati Mkurugenzi alishaomba msamaha makosa hayatajirudia tena katika vikao vingine.


Naye Diwani wa Kata ya Ilala Saddy Kimji ameomba Serikali iwalete Tarula kama kweli Wapo waweze kushiriki Vikao vya baraza la madiwani  Ilala  na kufahamu changamoto zilizopo za barabara za halmashauri.


Diwani Saddy alisema ni aibu ndani ya manispaa yao ambayo IPO Jirani na sura ya nchi yaani IKULU lakini barabara mbovu.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilala Dkt.Victoria Ludovick alisema  Manispaa inatenga fedha katika bajeti ijayo ili kila kata waweze kutoa matibabu kwa wananchi bure .


Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL