MWENYEKITI AWATAKA WAKAZI WA MJI MPYA KUSIMAMISHA UJENZI MPYA.

 Na Mwandishi Wetu.

MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa Mtongani Kata ya Kunduchi Richard Rusisye  amewataka wakazi wa Mji Mpya kuacha kuendeleza   ujenzi holela wasubiri utaratibu kutoka kwa  Maofisa wa Mipango Miji ili waweze kujenga makazi bora.

Hayo aliyasema jijini Dar es Salaam hivi karibuni  Mwenyekiti  wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa habari kuhusu changamoto mbalimbali zilizopo kwenye mtaa wake.

Mwenyekiti Richard Rusisye alisema changamoto kwenye mtaa  wa Mtongani  ni ujenzi holela  hasa Mtaa wa Mji Mpya ambapo wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakijenga nyumba mpya bila kufuata utaratibu wa Mipango Miji.

“Wakazi wa eneo la Mji Mpya wasimamishe ujenzi mpya wa nyumba ili kutoa fursa ya kutoa picha ya Mtaa huo kwa  Maofisa wa Mipango Miji  hadi pale  watakapokuja  kupima maeneo hayo, kwani utaratibu unafanyika ili kuja kupanga vema Mtaa huu,”alisema

Pamoja na Mwenyekiti Richard Rusisye kutoa agizo  hilo la ujenzi mpya kusimamishwa lakini bado wakazi wa eneo hilo wameendelea na ujenzi.

Hata hivyo Mwenyekiti Richard Rusisye  alizungumzia suala la usafi wa Mazingira  katika mtaa wake alisema mtu yeyote asiyefanya usafi atatozwa faini ya Shilingi 50,000.

“Mtu yeyote asiyefanya usafi wa mazingira atalipa faini ya Shilingi 50,000 na Askari wangu wa Ulinzi Shirikishi wanazungukia mitaani kwaajili ya kudhibiti usafi wa mazingira atakayebainika kwa hili hatutakuwa na huruma naye,”alisema Mwenyekiti.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo alizungumzia changamoto mbalimbali zilizopo kwenye mtaa wake ikiwamo Ulinzi Shirikishi ambapo wamejipanga kuboresha ili kupunguza wizi mdogo mdogo uliopo kwenye mtaa.
 MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa Mtongani Kata ya Kunduchi Richard Rusisye , akimuingia mmoja wa wafanyabiashara wa ndizi na viazi eneo la Mji  Meko ambako Serikali ya Mtaa ilitoa  eneo hilo la wazi kwaajili ya fursa  kwa wafanyabiashara wadogo wadogo.
 MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa Mtongani Kata ya Kunduchi Richard Rusisye  akiendelea kumuonyesha Mwandishi wa Habari maeneo ambayo Serikali ya Mtaa imetoa kwaajili ya wafanyabiashara wadogo wadogo.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL