MWENYEKITI WA CCM ALITUPIA LAWAMA JESHI LA POLISI.

 Mfanyakazi wa Mk Guest, Josephine Simon alionesha majera aliyofinywa na wanaodaiwa kuwa ni askari polisi.

Mwenyekiti wa CCM  Kata ya Kiwalani, Mathias Kahinga akizungumza na wanahabari hawapo pichani baada ya kuzungumza na mkuu wa polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni jana jijini Dar es Salaam.



Leonce Zimbandu

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Kata ya Kiwalani,Mathias Kahinga amelitupia lawama Jeshi la Polisi nchini kwa  kutumia silaha kuwakamata wateja wanne na mfanyakazi mmoja wa kike.

 Novemba 27, 2017 askari 10 waliovaa kiraia walifika katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo MK guest iliyopo Mtaa wa Kigilagila wakiwa na silaha za moto kwa  kuwakamata na wengine kufinywa.

Kahinga aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuonana na Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni jijini Dar es Salaam jana.

Alisema hakubaliani na kitendo cha kihuni kilichofanywa na askari hao kwa vile yeye ni kiongozi wa Kata anawajibu wa kusimamia serikali katika eneo hilo, hivyo alipaswa kuelezwa tatizo baada ya ukamataji huo.

“Inashangazwa eneo langu la biashara linavamiwa askari bila taarifa na kuwafanya wageni wengi kuhama, hali hiyo inafanya biashara kuwa ngumu kwa hofu ya kukamatwa,” alisema.

Mikidadi Mohamed ni mmoja wa wageni waliokamatwa alisema kuwa yeye alikamawa wakati akitoka chumbani kwenda nje na kukutana na askari hao na kumkamata.

Alisema alipojaribu kuuliza kosa lake la kukamatwa ni nini, walimjibu kuwa atajuulisha baada ya kufika katika kituo kidogo cha polisi cha Yombo Mama.

“Nimeshangaa hata nilipofikishwa katika kituo hicho sikuelezwa kosa bali waliniweka ndani kwa saa mbili na kasha kunipeleka kituo cha Buguruni na kutolewa jioni kwa faini,” alisema.

Mfanyakazi wa usafi wa guest hiyo, Josephine Simon alisema kuwa yeye ameshangazwa na kudhalilishwa na askari wa kiume kwa kunifinya na kuniachia majeraha kwenye mwili wangu.

Alisema  hakufurahishwa na kitendo cha askari hao kufika  na kuanza kuwakamata wateja waliofikia katika nyumba ya kulala wageni.

“Unajua waliniburuza kutoka ndani ya guest hadi kwenye gari, huku wengine wakinifinya kwenye mikono yangu na kuniachia alama hadi sasa,” alisema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alisema kuwa Jeshi hilo limepokea malalamiko hayo na wanaendelea na uchunguzi ili kubaini kama taratibu zilikiukwa.

“Tukithibitisha kama taratibu hazikufuatwa askari waliohusika watachukuliwa hatua lakini askari yeyote anaruhusiwa kutekelezwa wajibu wake kwa mujibu wa sheria,” alisema.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL