MWITIKIO MDOGO WA MIKUTANO UNAVYOKWAMISHA ULINZI NA USALAMA KWENYE MITAA.


Na  Mwandishi Wetu.

MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Salasala Kata ya Wazo Hashim Semboja amesema mwitikio mdogo wa wananchi kwenye vikao vya mitaa kunachangia kutotatuliwa kwa tatizo la Ulinzi Shirikishi.

Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na mwandishi wa habari ofisini kwake juu ya  changamoto mbalimbali zilizopo  kwenye mtaa wake ambapo alisema changamoto kubwa ni Ulinzi na Usalama.

“Tangu tuingie madarakani tumekutana na changamoto moja kubwa ya Ulinzi na Usalama ambapo kuna matukio mengi ya wizi yalikuwa yanatokea ikiwamo ya  watu kuibiwa kwenye Baa zao pamoja na kuuawa kwa risasi,” alisema na kuongeza

“ Lakini ukiitisha mkutano  wananchi  hawaipi uzito na  tumefanya mikutano sita  ya Ulinzi na Usalama kwa kila zone  ila muitikio ni mdogo sana pia itikadi za vyama vya siasa zinachangia  pia wananchi kutounga mkono Ulinzi na Usalama,”
Hata hivyo Semboja alisema pamoja na changamoto hizo wamefanikiwa kupata fedha kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo zaidi ya Shilingi  Milioni  5, 000,000  kwaajili ya kuendeleza ujenzi wa Kituo cha Polisi ili kuimarisha zaidi usalama kwenye mtaa huo.

Pia alisema Ofisi ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee itachangia Shilingi  Milioni 10,000,000  kwaajili ya kuenzeka kituo hicho.

Semboja aliwashukuru wananchi pamoja na wadau mbalimbali wapenda maendeleo walioweza kuchangia fedha hizo kwaajili ya kumalizia kituo hicho ambapo kukamilika kwa kituo hicho kutasaidia kuimarisha Ulinzi na Usalama kwenye mtaa wao.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL