WAKRISTO WASHAURIWA JINSI YA KUPELEKA MAOMBI MBELE ZA MUNGU.



 Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life  lililopo Tegeta Nyuki, Eliya Peter , akifungua watu waliofungwa katika vifungo mbalimbali ikiwamo magonjwa na shida mbalimbali jana katika semina ya Maombi iliyofanyika  Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego iliyoanza jana 20 Desemba 2017 jijini Dar es Salaam.

 Watu wakiendelea kufunguliwa katika vifungo mbalimbali na kupokea Unabii kwa Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life  Eliya Peter, katika semina ya maombi  inayoendelea katika  Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego.

 Waumini wa Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego, walioshiriki semina ya Maombi iliyoanza jana.

 Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life  lililopo Tegeta Nyuki, Eliya Peter, akiendelea kuwaombea watu wenye shida mbalimbali walioshiriki kwenye semina hiyo, iliyofanyika Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego.

 Baadhi ya waumini walioshiriki semina hiyo jana katika Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego, iliyofunguliwa na Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life  lililopo Tegeta Nyuki, Eliya Peter. 

 Baadhi ya waumini wakiendelea kufuatilia mafunzo ya semina hiyo ya Maombi  inayofanyika katika Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego .

 Baadhi ya waumini wakiendelea kufuatilia mafunzo ya semina hiyo iliyofanyika jana Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego.

  Rev Joseph Marego  wa  Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT, akimkaribisha Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life   Eliya Peter  (hayupo pichani) kwaajili ya kufungua semina ya Maombi iliyoanza jana kwenye Kanisa hilo.


Mke wa  Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life,  Eliya Peter kushoto na kulia ni Mke wa Rev. Joseph Marego.

 Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life  lililopo Tegeta Nyuki, Eliya Peter , akiendelea kuwafungua watu waliofungwa kwenye vifungo mbalimbali.
Enles Mbegalo

ASILIMIA 70 ya Wakristo hawapeleki maombi mbele za Mungu ila wanapeleka malalamiko.

Hayo yalisemwa  na Mtumishi wa Mungu  na Nabii wa Kanisa la Christian Life  lililopo Tegeta Nyuki, Eliya Peter wakati akifungua  semina ya Maombi  katika Kanisa la Tabata Kimanga  EAGT kwa Rev Joseph Marego iliyoanza jana 20 Desemba 2017 jijini Dar es Salaam.

Alisema Wakristo kama wana wa Mungu huwasiliana na Mungu kwa njia ya maombi kwa kuwa maombi ni njia pekee ya kufanya Mungu aseme nao.

“Maombi ni njia pekee ya  kupeleka hitaji lako mbele za Bwana ila Wakristo hawapeleki maombi mbele za Mungu ila wanapeleka malalamiko,”alisema

Pia aliwataka Wakristo kutenga muda kwaajili ya maombi  kwani Maombi unayoombwa leo yanaweza yakawa jambo la kumkumbusha Mungu hitaji lako la kesho.

“Kitabu cha Wafilipi  4: 6….. Msijisumbue kwa neno lolote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, Haja zenu na zijulikane na Mungu  na katika Kitabu cha 1 Wathesalonike 5: 17…..Ombeni bila kukoma,”.

Mtumishi wa Mungu  na Nabii  Eliya Peter, aliwataka Wakristo kuwa  waombaji na sio kuombewa.


“Jifunze kuingia magotini wewe kama wewe tatizo la watu wengi wanaomba lakini hawaamini  wanachoomba kama kitatokea, Kitabu cha Marko 11: 24 ….Kwa sababu hiyo nawaambia Yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea , nayo yatakuwa yenu,”

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL