WANANCHI WAELEZEA JINSI GLOBAR MINING ALIVYOWAVUNJIA NYUMBA ZAIDI YA 50.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Salasala Kata ya Wazo, Hashimu
Semboja kulia aliyeyevaa tisheti nyeupe, kulia ni Jakson Kakiziba
akibishana na Mwenyekiti juu ya wananchi kwenda kusafisha eneo hilo.
Jakson Kakiziba kushoto
katikati ni Mwandishi wa Habari wa Chanel Ten Fred Mwanjala na kulia ni mtoto
wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Mining Jerry Kakiziba ambao walifika eneo hilo baada ya
wananchi kuanza kusafisha.
Baadhi ya wananchi ambao walibomolewa nyuza hizo mwaka 2010
na Kampuni ya Global Mining
inayomilikiwa na Jerry Kakiziba, wakisafisha eneo hilo.
Wananchi waliobomolewa nyumba zao wakiendelea kufyeka eneo hilo, lengo ni kurudi kwenye eneo hilo.
Mtoto wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Mining inayomilikiwa na Jerry Kakiziba akiwa
amesimama akishuhudia kinachoendelea kwenye eneo hilo, pembeni yake ni lori
linalochukua kokoto kwenye eneo ambalo Serikali ilishafunga machimbo hayo tangu
2006.
Baadhi ya wananchi waliofika eneo hilo jana.
Wananchi wakiwa wamesimama wakishuhudua kinachoendelea hapo, huku wakiendelea kutoa malalamiko juu ya Kampuni ya Global Mining kwa kitendo ambacho amekuwa wakiwafanyia wananchi hao.
Baadhi ya wananchi wakishuhudia kinachoendelea, nyuma yao ni moja ya nyumba ambayo Mkurugenzi wa Kampuni hiyo alijimilikisha baada ya kubomoa nyumba zote.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Salasala Kata ya Wazo,
Hashimu Semboja , aliyevaa tisheti jeupe akiwa na baadhi ya wananchi waliofika eneo hilo.
Wananchi wakiondoka kwenye eneo hilo jana.
Na Mwandishi Wetu.
WAKAZI wa Salasala Mtaa wa Luona wameelezea jinsi Kampuni ya Globar Mining
inayomilikiwa na Jerry Kakiziba ilivyowanyanyasa na kuwavunjia nyumba zaidi ya
50 na kuwanyanganya eneo lao.
Aidha, wameiomba Serikali kupitia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul
Makonda kuwasaidia kutatua mgogoro huo
wa ardhi kama alivyosaidia maeneo
mengine .
Wakizungumza na waandishi wa habari jana wakazi hao
ambao walienda kufyeka eneo hilo kwa lengo la kurudi kwenye eneo lao walisema hawana sehemu ya
kuishi na hivyo wanalazimika kurudi katika
eneo ambao lilikuwa ni makazi yao.
Naye, Matheo Haule
alisema wao walikuwa wachimbaji
wadogo kwenye eneo hilo ila baada ya Serikali kufunga machimbo hayo 2006 waligawana viwanja hivyo na kujenga
nyumba zao.
Alisema baada ya kujenga nyumba zao Kampuni ya
Glober Mining ambaye naye alikuwa miongoni mwa Makampuni makubwa yaliyokuwa
yakichimba machimbo maeneo hayo ilienda
na kuvamia eneo hilo mwaka 2010 na kuvunja nyumba zao.
“Baada ya Serikali kufunga machimbo haya ya kokoto
mwaka 2006 sisi tuligawana viwanja eneo ambalo tulikuwa tunachimba na kujenga nyumba, lakini mwaka
2010 Kampuni ya Glober Mining ilikuja na kuvamia eneo letu na kutuvunjia nyumba
zaidi ya 50,”alisema Haule na kuongeza
“Mmiliki
huyu licha ya kutubomolea nyumba ameendelea kutoa
vitisho kwetu na kutunyanyasa kwa
kutumia nguvu za dola kila tunapotaka kurudi kwenye eneo,”
Alisema pamoja na kuvunja nyumba zote hizo na
kubakisha nyumba moja ambayo “Ilikuwa nyumba yangu na anaendelea kuitumia kwa
kuwahifadhi ndugu zake ambao wamekuwa wakilinda eneo hili,”
Abdara Njole, alisema wanaiomba Serikali iingilie
kati kwani Nchi hii bado ina mabepari
wakubwa na wanao nyanyasa wananchi walio
katika hali ya chini kwa kutumia fedha
zao.
“Huyu bwana ni mtu maarufu Serikalini na ni mtu
mwenye fedha nyingi sana na anauwezo wa kukukamata na kukubambikia kesi na huwa
anatwambia tutakapo rudi hapa sisi tutakuwa halali yake kwa chochote kitakachotokea,”
Paulo Pasco alisema
Mkurugenzi huyo amekuwa akiwaambia kuwa Serikali ameiweka
mikononi na hakuna ofisi ambayo itawasikiliza wao kwani ofisi zote zimejaa
Wahaya na Wahaya wote ni ndugu zake.
Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Salasala Kata ya
Wazo, Hashimu Semboja alisema mgogoro huo aliukuta baada ya kuingia madarakani
2015 .
Alisema wananchi hao walipeleka malalamiko kwenye
ofisi yake na kumueleza jinsi Kampuni hiyo ilivyowabomolea nyumba zao na baada
ya malalamiko hayo aliamua kujiridhisha.
Alisema
hakuishia hapo aliendelea kufuatilia suala hilo kwenye ngazi za juu ili
kujiridhisha zaidi Mmiliki halali wa eneo hilo ila alibaini kuwa Globar Mining
sio Mmiliki wa eneo hilo ila alikuwa na kibali cha kuchimba na sio kumiliki
ardhi.
“Mimi nashangazwa sana uhalali wa Globar Mining uko
wapi, huyu mtu ni mbabaishaji akiambiwa alete vielelezo vya umiliki wa eneo
hili anasema anaendelea kushughurikia vielelezo,”alisema Semboja
“Hii sehemu sio yake ilikuwa ya wachimbaji wadogo lakini baada ya Serikali
kufunga machimbo haya mwaka 2006
makampuni makubwa yaliondoka, ila Kampuni ya Globar Mining ilibaki na kuendelea
kuchimba,”alisema
“ Eneo lake ni
lile kule nyumba ambalo alikuwa akilitumia kabla machimbo hayajafungwa ila alivamia
eneo walilokuwa wakitumia wachimbaji wadogo na kuwavunjia nyumba zao,”
“ Baada ya kufuatilia na kujua ukweli juu ya eneo
hili nilimuandikia barua aje Ofisi ya Serikali ya Mtaa kujieleza juu ya
unyanyasaji anaoendelea kuufanya kwa wanachi ambao aliwabomolea nyumba zao ila
cha kushangaza alitujibu kwa kutuma onyo juu ya kufuatilia suala hili,”
Alisema eneo hilo lingeweza kutumika kwaajili ya
kujenga huduma za jamii ikiwamo Soko, Ofisi ya Serikali ya Mtaa, Shule na
Hospitali kwani mtaa wake hauna huduma
za kijamii na pia lingetolewa kwaajili ya wale wananchi 51ambao walivunjiwa
nyumba zao na Globar Mining.
Pia Mwenyekiti alilalamikia kitendo cha Kampuni hiyo
kuendelea kuchimba mawe kinyume na sheria kwenye eneo hilo ambalo Serikali ilishafunga tangu
mwaka 2006 na uchimbaji huo umekuwa ukiwaletea athari watoto wadogo na wengine wamekuwa wakipoteza
maisha.
Hata hivyo mmoja wa wadogo wa Mkurugenzi wa Kampuni
hiyo ambaye alijitambulisha kwa jina la Jakson Kakiziba alisema eneo hilo
wanalimiliki kihalali na wana nyaraka zote za umiliki wa eneo hilo.
Comments
Post a Comment