WAZEE ZINGIZIWA WAOMBA RAIS AWAKUMBUKE.

Kamati ya mipango na fedha Kikundi cha Wazee Amani Group wakimsikiliza mwalimu wa ujasiliamali (Hayupo pichani) alipowatembelea hivi karibuni.


 wa Kikundi cha Wazee Amani Group wakimsikiliza mwalimu wa ujasiliamali (Hayupo pichani) alipowatembelea hivi karibuni.

Wanakikundi cha Wazee wa Amani Group wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya mafunzo ya ujasiliamali.



Leonce Zimbandu.

KIKUNDI cha Wazee Amani Group (WAG) kilichopo Kata ya Zingiziwa Manispaa ya Ilala, kimemuomba Rais John Magufuli kuwakumbuka na kuwaita kwenye mikutano ya Wazee wa Mkoa wa  Dar es Salaam.

Ombi hilo limetolewa na wazee hao baada ya kufanya usajili kikundi chao mwaka 2002 kwa namba 337 na kukabidhiwa  cheti chenye kumb. namba 19238 kwa lengo la kutetea haki za wazee wa Tanzania, Afrika na Ulimwenguni kote.

Mwenyekiti wa kikundi cha WAG, Msahilo Mbegu aliyasema hayo alipokuwa akizungumza kwa uchungu na waandishi wa habari waliowatembelea hivi karibuni ili kujua changamoto zinazowakabili.

Alisema haelewi utaratibu unaotumika kuwatambua wazee wa kukutana na Rais bila hata kikundi chao ambacho  kilichosajiliwa kisheria kupata mwaliko wa kuhudhuria hata mtu mmoja.

“Tunaishukuru  serikali kututambua rasmi kwa  kuunda wizara inayotushughulikia matatizo yetu lakini tunahitaji huduma za msingi zipatikane kwenye vituo vya afya,” alisema.

  Alisema  wazee wanachangamoto nyingi, ikiwamo afya (bima), chakula na malazi kwa vile wengine hawana  watu wa kuwasaidia, hivyo kikundi hicho kimeanzishwa kwa lengo la  kuwasaidia wengine.

Aliongeza kuwa iwapo serikali itawaunga mkono kwa kuwaunganisha na kikundi cha wazee waliopo nchini  Afrika ya Kusini watafurahi ili wabadilishana nao uzoefu wa namna ya kuendesha vikundi hivyo.


Kufuatia hatua hiyo iliyochukuliwa na wazee hao kukaa pamoja na kuunda umoja huo ni jambo la kuwapongeza na serikali inapaswa kuongeza nguvu ili kuwapatia nyenzo za kujikimu.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL