WIZARA YA AFYA YAZUIYA LIKIZO KWA MADAKTARI NA WAUGUZI.


Na Heri Shaaban

NAIBU WAZIRI wa Afya na Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Dkt, Faustine Ndugulile ameziagiza Halmashauri kuangalia upya utoaji wa likizo kwa Madaktari na Wauguzi katika kipindi cha kufunga mwaka kutokana na idadi ya wagonjwa kuwa kubwa .


Dkt .Ndungulile alisema hayo Wilayani Ilala katika vituo vya afya alivyotembelea jimboni Segerea  ambavyo ni Buguruni Plani ,Tabata A na segerea Ugombolwa .

" Kipindi cha mwisho wa mwaka kina changamoto kwa upande wa wagonjwa wanakuwa wengi, hivyo kabla ya kuwapa rikizo taratibu za utoaji zifuatwe lengo wagonjwa waweze kupata huduma kwa wakati" alisema Ndungulile.
 Katika ziara yake ameweza kujionea idadi ya wagonjwa wengi wakisubiri matibabu katika vituo vya afya alivyotembelea   katika ziara yake hiyo ya kikazi.

Aidha katika hatua nyingine  Naibu Waziri Ndungulile  amepiga marufuku  wagonjwa kuandikiwa kununua dawa  nje ya vituo vya afya vya serikali badala yake wagonjwa wote  wapewe dawa katika vituo hivyo  vya serikali kwani imenunua dawa za kutosha.

Aliwakikishia wananchi Wizara imeshasambaza dawa katika vituo vya afya nchi nzima  lengo kuwapa huduma bora.

Wakati huohuo ametoa muda wa miezi mitatu Manispaa ya Ilala kuboresha mfumo wa Mapato na Maabara katika Hospitali ya Plani iliyopo Buguruni Mnyamani.
Kwa upande wake Mbunge wa Segerea (CCM) Bonah Kaluwa amemuomba Naibu Waziri  kuongea na Serikaki Kuu ili kuarakisha Wakala wa Barabara TARURA kujenga Barabara ya Mnyamani ili wagonjwa wafike kwa wakati kupatiwa matibabu.

"Kilio changu barabara ya Mnyamani wananchi wangu wanapata shida njia mbovu muda mrefu mpaka sasa hakuna hatua zilizochukuliwa  gari la wagonjwa pia linapita kwa shida kupeleka wagonjwa wa rufaa "alisema Kaluwa.

Pia aliomba Wizara kuipandisha hadhi zahanati hiyo ya Plani .


Naye Dkt. wa Zamu  Msimamizi wa  Vitendo Neema Ntabaye alisema madktari waliopo 12  wana kabiliana na changamoto  ya jengo la upasuaji.

Comments

Popular posts from this blog

ASKOFU MWAMAKULA AMUWEKA WAKFU ASKOFU MPYA KENYA.

NABII ELIYA AZIDI KUFUNGUA WATU WALIOFUNGWA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA NA MFALME WA DUBAI, WAFANYABIASHARA, ATEMBELEA BANDARI WA JEBEL ALI PORT NA KUTEMBELEA MRADI WA AKHEEL